Kum. 14:10-20 Swahili Union Version (SUV)

10. na kila kisichokuwa na mapezi na magamba msile; ni najisi kwenu.

11. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.

12. Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;

13. na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;

14. na kila kunguru kwa aina zake;

15. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;

16. na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;

17. na mwari, na nderi, na mnandi;

18. na membe, na koikoi, kwa aina zake; na hudihudi, na popo.

19. Na wadudu wote watambaao wenye mabawa ni najisi kwenu; msiwale.

20. Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.

Kum. 14