Kum. 14:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Ninyi mmekuwa wana wa BWANA, Mungu wenu; msijitoje miili yenu, wala msifanye upaa katikati ya macho yenu kwa ajili ya aliyekufa.

2. Kwa kuwa u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako, na BWANA amekuchagua kuwa watu wake hasa, kuliko mataifa yote yaliyo juu ya uso wa nchi.

3. Usile kitu cho chote kichukizacho.

4. Wanyama mtakaokula ni hawa ng’ombe, na kondoo, na mbuzi,

5. kulungu, na paa, na kongoni, na mbuzi wa mwitu, na paa mweupe, na pofu, na mbuzi wa mlima;

Kum. 14