Isa. 7:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Kwa maana kichwa cha Shamu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini; na katika muda wa miaka sitini na mitano Efraimu atavunjika vipande vipande, asiwe kabila ya watu tena;

9. tena kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia. Kwamba hamtaki kusadiki, bila shaka hamtathibitika.

10. Tena BWANA akasema na Ahazi akinena,

11. Jitakie ishara ya BWANA, Mungu wako; itake katika mahali palipo chini sana, au katika mahali palipo juu sana.

12. Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu BWANA.

Isa. 7