1. Na nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu katika habari za shamba lake la mizabibu.Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu,Kilimani penye kuzaa sana;
2. Akafanya handaki kulizunguka pande zote,Akatoa mawe yake,Akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri,Akajenga mnara katikati yake,Akachimba shinikizo ndani yake;Akatumaini ya kuwa utazaa zabibu,Nao ukazaa zabibu-mwitu.
3. Na sasa, enyi wenyeji wa Yerusalemu, nanyi watu wa Yuda, amueni, nawasihi, kati ya mimi na shamba langu la mizabibu.