Isa. 45:10-12 Swahili Union Version (SUV)

10. Ole wake amwambiaye baba yake, Wazaa nini? Au mwanamke, Una utungu wa nini?

11. BWANA, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni.

12. Mimi nimeiumba dunia, nimemhuluku mwanadamu juu yake; Mimi, naam, mikono yangu mimi, imezitanda mbingu, na jeshi lake lote nimeliamuru.

Isa. 45