Isa. 44:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Lakini sikia sasa, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua;

2. BWANA, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.

3. Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;

4. nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.

5. Mmoja atasema, Mimi ni wa BWANA; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa BWANA, na kujiita kwa jina la Israeli.

Isa. 44