Isa. 33:7-10 Swahili Union Version (SUV)

7. Angalia, mashujaa wao wanalia nje, wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.

8. Njia kuu zimeachwa, msafiri amekoma; ameyavunja maagano, ameidharau miji, hamjali mtu.

9. Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani.

10. Basi, sasa nitasimama; asema BWANA; sasa nitajiinua, sasa nitajitukuza.

Isa. 33