Isa. 33:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Kabila za watu wamekimbia wakisikia kelele za fujo; mataifa wametawanyika ulipojiinua nafsi yako.

4. Na mateka yako yatakumbwa kama wadudu wakumbavyo, wataruka juu yake kama arukavyo nzige.

5. BWANA ametukuka; kwa maana anakaa juu; amejaza Sayuni hukumu na haki.

6. Nyakati zako zitakuwa nyakati za kukaa imara; za wokovu tele na hekima na maarifa; kumcha BWANA ni hazina yake ya akiba.

Isa. 33