6. Mguu utaukanyaga chini,Naam, miguu yao walio maskini,Na hatua zao walio wahitaji.
7. Njia yake mwenye haki ni unyofu;Wewe uliye mnyofu wainyosha njia ya mwenye haki.
8. Naam, katika njia ya hukumu zakoSisi tumekungoja, Ee BWANA;Shauku ya nafsi zetu inaelekeaJina lako na ukumbusho wako.
9. Kwa nafsi yangu nimekutamani wakati wa usiku;Naam, kwa nafsi yangu ndani yangu nitakutafuta mapema;Maana hukumu zako zikiwapo duniani,Watu wakaao duniani hujifunza haki.
10. Mtu mbaya ajapofadhiliwa,Hata hivyo hatajifunza haki;Katika nchi ya unyofu atatenda udhalimu,Wala hatauona utukufu wa BWANA.
11. BWANA, mkono wako umeinuliwa, lakini hawaoni; lakini watauona wivu wako kwa ajili ya watu wako, nao watatahayari; naam, moto utawala adui zako.
12. BWANA, utatuamuria amani; maana ni wewe pia uliyetutendea kazi zetu zote.
13. Ee BWANA, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametumiliki; lakini kwa msaada wako peke yako tutalitaja jina lako.
14. Wao wamekufa, hawataishi; wamekwisha kufariki, hawatafufuka; kwa sababu hiyo umewajilia, na kuwaangamiza, na kuupoteza ukumbusho wao.
15. Umeliongeza hilo taifa, BWANA, umeliongeza taifa; wewe umetukuzwa, umeipanua mipaka yote ya nchi hii.