Isa. 2:12-17 Swahili Union Version (SUV)

12. Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.

13. Na juu ya mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu na kuinuka, na juu ya mialoni yote ya Bashani;

14. na juu ya milima mirefu yote, na juu ya vilima vyote vilivyoinuka;

15. na juu ya kila mnara mrefu, na juu ya kila ukuta ulio na boma;

16. na juu ya merikebu zote za Tarshishi, na juu ya kila taswira ipendezayo.

17. Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.

Isa. 2