12. Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.
13. Na juu ya mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu na kuinuka, na juu ya mialoni yote ya Bashani;
14. na juu ya milima mirefu yote, na juu ya vilima vyote vilivyoinuka;
15. na juu ya kila mnara mrefu, na juu ya kila ukuta ulio na boma;
16. na juu ya merikebu zote za Tarshishi, na juu ya kila taswira ipendezayo.
17. Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.