17. Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake;Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?
18. Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima,Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;
19. Bali wewe umetupwa mbali na kaburi lako,Kama chipukizi lililochukiza kabisa;Kama vazi la wale waliouawa,Wale waliochomwa kwa upanga,Wale washukao mpaka misingi ya shimo;Kama mzoga uliokanyagwa chini ya miguu.
20. Hutaungamanishwa pamoja nao katika mazishi,Kwa maana umeiharibu nchi yako,Umewaua watu wako;Kizazi chao watendao uovu hakitatajwa milele.
21. Fanyeni tayari machinjo kwa watoto wake.Kwa sababu ya uovu wa baba zao;Wasije wakainuka na kuitamalaki nchi,Na kuujaza miji uso wa ulimwengu.
22. Nami nitainuka, nishindane nao; asema BWANA wa majeshi; na katika Babeli nitang’oa jina na mabaki, mwana na mjukuu; asema BWANA.