4. Na katika siku hiyo mtasema,Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa,Litajeni jina lake kuwa limetukuka.
5. Mwimbieni BWANA; kwa kuwa ametenda makuu;Na yajulikane haya katika dunia yote.
6. Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni;Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.