1. Haya ni maono ya Isaya, mwana wa Amozi, aliyoyaona katika habari za Yuda na Yerusalemu, siku za Uzia na Yothamu na Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.
2. Sikieni, enyi mbingu, tega sikio, Ee nchi, kwa maana BWANA amenena;Nimewalisha watoto na kuwalea, nao wameniasi.
3. Ng’ombe amjua bwana wake,Na punda ajua kibanda cha bwana wake;Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.
4. Ole wake, taifa lenye dhambi, watu wanaochukua mzigo wa uovu, wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu; wamemwacha BWANA, wamemdharau yeye aliye Mtakatifu wa Israeli, wamefarakana naye na kurudi nyuma.