5. Naam, BWANA, Mungu wa majeshi;BWANA ndilo kumbukumbu lake.
6. Basi, mrudie Mungu wako; shika fadhili na hukumu; ukamngojee Mungu wako daima.
7. Ni mchuuzi, mizani ya udanganyifu i mkononi mwake; anapenda kudhulumu.
8. Naye Efraimu alisema, Kweli nimekuwa tajiri, nimejipatia mali nyingi; katika kazi zangu zote hawataona kwangu uovu wo wote uliokuwa dhambi.