22. Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
23. Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, Hivi ndivyo mtakavyowabarikia wana wa Israeli; mtawaambia;
24. BWANA akubarikie, na kukulinda;
25. BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
26. BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.
27. Ndivyo watakavyoweka jina langu juu ya wana wa Israeli; nami nitawabarikia.