Hes. 4:20-24 Swahili Union Version (SUV)

20. lakini wasiingie wao kupaona mahali pale patakatifu, hata kwa dakika moja, ili wasife.

21. Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia,

22. Fanya jumla ya wana wa Gershoni nao, kwa nyumba za baba zao, na jamaa zao;

23. tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini utawahesabu; wote watakaoingia kutumika, ili kufanya kazi katika hema ya kukutania.

24. Huu ni utumishi wa jamaa za Wagershoni, katika kutumika na katika kuchukua mizigo;

Hes. 4