5. Basi Musa akaleta neno lao mbele ya BWANA
6. BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
7. Hao binti za Selofehadi wananena lililo haki; kweli utawapa milki ya urithi pamoja na ndugu za baba yao; nawe utawapa urithi wa baba yao.
8. Kisha utanena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Mtu akifa, naye hana mwana wa kiume, ndipo utampa binti yake urithi wake.
9. Tena ikiwa hana binti, mtawapa nduguze urithi wake.