5. BWANA akatia neno katika kinywa chake Balaamu, akasema, Umrudie Balaki; ukaseme maneno haya.
6. Akarudi kwake, na tazama, amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, yeye na wakuu wote wa Moabu pamoja naye.
7. Akatunga mithali yake, akasema,Balaki amenileta kutoka Aramu,Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki,Njoo! Unilaanie Yakobo,Njoo! Unishutumie Israeli.
8. Nimlaanije, yeye ambaye Mungu hakumlaani?Nimshutumuje, yeye ambaye BWANA hakumshutumu?