18. Naye akatunga mithali yake, akasema,Ondoka Balaki, ukasikilize;Nisikilize, Ee mwana wa Sipori;
19. Mungu si mtu, aseme uongo;Wala si mwanadamu, ajute;Iwapo amesema, hatalitenda?Iwapo amenena, hatalifikiliza?
20. Tazama, nimepewa amri kubariki,Yeye amebariki, nami siwezi kulitangua.
21. Hakutazama uovu katika Yakobo,Wala hakuona ukaidi katika Israeli.BWANA, Mungu wake, yu pamoja naye,Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao.
22. Mungu amewaleta kutoka Misri,Naye ana nguvu kama nguvu za nyati.