15. Na matelemko ya hizo bondeKwenye kutelemkia maskani ya Ari,Na kutegemea mpaka wa Moabu.
16. Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho BWANA alimwambia Musa, Uwakutanishe watu, nami nitawapa maji.
17. Ndipo Israeli wakaimba wimbo huu;Bubujika Ee kisima; kiimbieni;
18. Kisima walichokichimba wakuu,Ambacho wakuu wa watu wakakifukua,Kwa fimbo za enzi, kwa fimbo zao.Kutoka lile jangwa wakaenda Matana;
19. na kutoka Matana wakaenda Nahalieli; na kutoka Nahalieli wakaenda Bamothi;
20. na kutoka Bamothi wakaenda bondeni kwenye konde la Moabu, hata kilele cha Pisga, kielekeacho chini jangwani.
21. Kisha Israeli akatuma wajumbe kumwendea Sihoni mfalme wa Waamori, na kusema,