Hes. 13:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,

2. Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.

3. Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na BWANA; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli.

4. Na majina yao ni haya; katika kabila ya Reubeni, Shamua mwana Zakuri.

5. Katika kabila ya Simeoni, Shafati mwana wa Hori.

Hes. 13