Hes. 11:9-11 Swahili Union Version (SUV)

9. Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao.

10. Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za BWANA zikawaka sana; Musa naye akakasirika.

11. Musa akamwambia BWANA, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu?

Hes. 11