45. Basi hao wote waliohesabiwa katika wana wa israeli kwa kuandama nyumba za baba zao tangu umri wa miaka ishirini na zaidi; wote walioweza kwenda vitani katika Israeli;
46. hao wote waliohesabiwa walikuwa ni watu waume mia sita na tatu elfu na mia tano na hamsini (603,550).
47. Lakini Walawi kwa kuiandama kabila ya baba zao hawakuhesabiwa katika watu hao.
48. Kwa kuwa BWANA alinena na Musa, na kumwambia,
49. Hiyo kabila ya Lawi tu usiihesabu, wala usiitie hesabu yao katika wana wa Israeli;