13. Ndipo Hagai mjumbe wa BWANA, katika ujumbe wa BWANA, akawaambia watu, akisema, Mimi nipo pamoja nanyi, asema BWANA.
14. BWANA akaiamsha roho ya Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na roho ya Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na roho zao mabaki ya watu; wakaenda, wakafanya kazi katika nyumba ya BWANA wa majeshi, Mungu wao;
15. katika siku ya ishirini na nne ya mwezi, katika mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa Dario mfalme.