Hab. 3:12-14 Swahili Union Version (SUV)

12. Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu;Ukawapura mataifa kwa hasira.

13. Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako,Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako;Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu,Ukiuweka wazi msingi hata mwambani.

14. Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe;Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya;Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri.

Hab. 3