Hab. 3:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Sala ya nabii Habakuki.

2. Ee BWANA, nimesikia habari zako, nami naogopa;Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka;Katikati ya miaka tangaza habari yake;Katika ghadhabu kumbuka rehema.

3. Mungu alikuja kutoka Temani,Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani.Utukufu wake ukazifunika mbingu,Nayo dunia ikajaa sifa yake.

4. Mwangaza wake ulikuwa kama nuru;Alikuwa na mishale ya nuru ubavuni pake;Ndipo ulipofichwa uweza wake.

5. Mbele zake ilikwenda tauni,Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake.

Hab. 3