1. Sala ya nabii Habakuki.
2. Ee BWANA, nimesikia habari zako, nami naogopa;Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka;Katikati ya miaka tangaza habari yake;Katika ghadhabu kumbuka rehema.
3. Mungu alikuja kutoka Temani,Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani.Utukufu wake ukazifunika mbingu,Nayo dunia ikajaa sifa yake.
4. Mwangaza wake ulikuwa kama nuru;Alikuwa na mishale ya nuru ubavuni pake;Ndipo ulipofichwa uweza wake.
5. Mbele zake ilikwenda tauni,Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake.