Eze. 1:17-19 Swahili Union Version (SUV)

17. Yalipokwenda yalikwenda pande zote nne; hayakugeuka yalipokwenda.

18. Katika habari za vivimbe vyake; vilikuwa virefu, vya kutisha; nayo yote manne, vivimbe vyake vimejaa macho pande zote.

19. Na viumbe hao walipokwenda, magurudumu yalikwenda kandokando yao, na viumbe hao walipoinuliwa, magurudumu nayo yaliinuliwa.

Eze. 1