2. siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote.
3. Nao maakida wa majimbo, na majumbe, na maliwali, na wale waliofanya shughuli ya mfalme, waliwasaidia Wayahudi; kwa sababu hofu ya Mordekai imewaangukia.
4. Maana Mordekai alikuwa mkuu nyumbani mwa mfalme, na sifa yake imevuma katika majimbo yote, kwa kuwa huyo Mordekai amezidi kukuzwa.
5. Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.
6. Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza.
7. Wakawaua na Parshandatha, na Dalfoni, na Aspatha,
8. na Poratha, na Adalia, na Aridatha,
9. na Parmashta, na Arisai, na Aridai, na Waizatha,
10. wana kumi wa Hamani bin Hamedatha, adui ya Wayahudi; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono.
11. Siku ile mfalme akaletewa hesabu ya hao waliouawa huko Shushani ngomeni.