Efe. 1:21-23 Swahili Union Version (SUV)

21. juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;

22. akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo

23. ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

Efe. 1