Ebr. 7:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Na hapa wanadamu wapatikanao na kufa hutwaa sehemu ya kumi; bali huko yeye ashuhudiwaye kwamba yu hai.

9. Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi;

10. kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye.

11. Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo); kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?

12. Maana ukuhani ule ukibadilika, hapana budi sheria nayo ibadilike.

Ebr. 7