Ebr. 13:6-8 Swahili Union Version (SUV)

6. Hata twathubutu kusema,Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa;Mwanadamu atanitenda nini?

7. Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.

8. Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.

Ebr. 13