6. Hata twathubutu kusema,Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa;Mwanadamu atanitenda nini?
7. Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.
8. Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.