3. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.
4. Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;
5. tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana,Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana,Wala usizimie moyo ukikemewa naye;
6. Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi,Naye humpiga kila mwana amkubaliye.
7. Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?
8. Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali.