11. Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.
12. Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;
13. tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake.
14. Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
15. Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema,
16. Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana,Nitatia sheria zangu mioyoni mwao,Na katika nia zao nitaziandika;ndipo anenapo,
17. Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
18. Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.