Dan. 10:13-15 Swahili Union Version (SUV)

13. Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.

14. Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.

15. Na alipokwisha kusema nami maneno hayo, nikauelekeza uso wangu chini, nikawa bubu.

Dan. 10