9. Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu, na Orioni, na hicho Kilimia,Na makundi ya nyota ya kusini.
10. Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana;Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11. Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone;Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue.
12. Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia?Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?