Ayu. 9:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Yeye afanyaye hizo nyota za Dubu, na Orioni, na hicho Kilimia,Na makundi ya nyota ya kusini.

10. Atendaye mambo makuu yasiyotafutikana;Naam, mambo ya ajabu yasiyohesabika.

11. Tazama, yuaenenda karibu nami, nisimwone;Tena yuapita kwenda mbele, nisimtambue.

12. Tazama, yuakamata, ni nani awezaye kumzuia?Ni nani awezaye kumwuliza, Wafanya nini?

Ayu. 9