11. Je! Hayo mafunjo yamea pasipo matopeNa makangaga kumea pasipo maji?
12. Yakiwa yakali mabichi bado, wala hayakukatwa,Hunyauka mbele ya majani mengine.
13. Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu;Na matumaini yake huyo mbaya huangamia;
14. Uthabiti wake utavunjika,Na matumaini yake huwa ni nyuzi za buibui.
15. Ataitegemea nyumba yake, isisimame;Atashikamana nayo, isidumu.
16. Yeye huwa mti mbichi mbele ya jua,Nayo machipukizi yake huenea katika bustani yake.