Ayu. 8:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. Je! Hayo mafunjo yamea pasipo matopeNa makangaga kumea pasipo maji?

12. Yakiwa yakali mabichi bado, wala hayakukatwa,Hunyauka mbele ya majani mengine.

13. Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu;Na matumaini yake huyo mbaya huangamia;

14. Uthabiti wake utavunjika,Na matumaini yake huwa ni nyuzi za buibui.

15. Ataitegemea nyumba yake, isisimame;Atashikamana nayo, isidumu.

16. Yeye huwa mti mbichi mbele ya jua,Nayo machipukizi yake huenea katika bustani yake.

Ayu. 8