11. Nguvu zangu ni zipi, hata ningoje?Na mwisho wangu ni nini, hata nisubiri?
12. Je! Nguvu zangu ni nguvu za mawe?Au mwili wangu, je! Ni shaba?
13. Je! Si kwamba sina msaada ndani yangu.Tena kwamba kufanikiwa kumeondolewa mbali nami?
14. Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki;Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi.
15. Ndugu zangu wametenda udanganyifu kama kijito cha maji.Mfano wa fumbi la vijito vipitavyo.