6. Kwani taabu haitoki mchangani,Wala mashaka hayachipuki katika nchi;
7. Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka,Kama cheche za moto zirukavyo juu.
8. Lakini mimi ningemtafuta Mungu,Ningemwekea Mungu daawa yangu;
9. Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana;Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;
10. Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi,Na kuyapeleka maji mashambani;
11. Awainuaye juu hao walio chini;Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.
12. Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu,Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.