2. Kwani hasira humwua mtu mpumbavu,Nao wivu humwua mjinga.
3. Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi;Lakini mara niliyalaani maskani yake.
4. Watoto wake wako mbali na wokovu,Nao wamesongwa langoni,Wala hapana atakayewaponya.
5. Mavuno yake wale wenye njaa huyala,Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani,Nao wenye kiu huzitwetea mali zao.
6. Kwani taabu haitoki mchangani,Wala mashaka hayachipuki katika nchi;
7. Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka,Kama cheche za moto zirukavyo juu.
8. Lakini mimi ningemtafuta Mungu,Ningemwekea Mungu daawa yangu;
9. Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana;Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu;
10. Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi,Na kuyapeleka maji mashambani;
11. Awainuaye juu hao walio chini;Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama.
12. Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu,Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao.