8. Mwekee mkono wako;Vikumbuke vile vita, wala usifanye tena.
9. Tazama, kumtamani ni bure;Je! Hatambwaga chini huyo atakayemtazama?
10. Hapana aliye mkali hata akathubutu kumwamsha;Bali ni nani awezaye kusimama mbele yangu mimi?
11. Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe?Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni changu.
12. Sitanyamaa kusema habari za via vyake,Wala nguvu zake kuu, wala umbo lake zuri.