24. Moyo wake una imara kama jiwe;Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.
25. Anapojiinua, mashujaa huogopa;Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.
26. Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii;Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.
27. Yeye huona chuma kuwa kama nyasi,Na shaba kama mti uliooza.
28. Mshale hauwezi kumkimbiza;Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.