Ayu. 41:24-28 Swahili Union Version (SUV)

24. Moyo wake una imara kama jiwe;Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia.

25. Anapojiinua, mashujaa huogopa;Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo.

26. Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii;Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.

27. Yeye huona chuma kuwa kama nyasi,Na shaba kama mti uliooza.

28. Mshale hauwezi kumkimbiza;Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi.

Ayu. 41