Ayu. 39:5-9 Swahili Union Version (SUV)

5. Ni nani aliyempeleka punda-milia aende huru?Au je! Ni nani aliyemfungulia vifungo punda-mwitu?

6. Ambaye nimeifanya nyika kuwa nyumba yake,Na nchi ya chumvi kuwa makao yake.

7. Yeye hudharau mshindo wa mji,Wala hasikii kelele zake msimamizi.

8. Upana wa milima ni malisho yake,Hutafuta-tafuta kila kitu kilicho kibichi.

9. Je! Nyati atakubali kukutumikia?Au atakaa katika zizi lako?

Ayu. 39