9. Nilipolifanya wingu kuwa vazi lake,Na giza zito kuwa nguo ya kuifungia,
10. Nikaiagiza amri yangu;Nikaiwekea makomeo na milango,
11. Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita,Na hapa mawimbi yako yanyetayo yatazuiliwa?
12. Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza?Umeyajulisha mapambazuko mahali pake?