Ayu. 38:9-12 Swahili Union Version (SUV)

9. Nilipolifanya wingu kuwa vazi lake,Na giza zito kuwa nguo ya kuifungia,

10. Nikaiagiza amri yangu;Nikaiwekea makomeo na milango,

11. Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita,Na hapa mawimbi yako yanyetayo yatazuiliwa?

12. Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza?Umeyajulisha mapambazuko mahali pake?

Ayu. 38