Ayu. 36:28-33 Swahili Union Version (SUV)

28. Ambayo mawingu yainyeshaNa kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.

29. Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu,Ngurumo za makao yake?

30. Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke;Naye hufunika vilindi vya bahari.

31. Kwani huwahukumu kabila za watu kwa njia hizi;Hutoa chakula kwa ukarimu.

32. Yeye huifunika mikono yake kwa umeme;Na kuuagiza shabaha utakayopiga.

33. Mshindo wake hutoa habari zake,Anayewaka hasira juu ya uovu.

Ayu. 36