Ayu. 36:24-30 Swahili Union Version (SUV)

24. Kumbuka kuitukuza kazi yake,Watu waliyoiimbia.

25. Wanadamu wote wameitazama;Watu huiangalia kwa mbali

26. Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui;Hesabu ya miaka yake haitafutiki.

27. Kwani yeye huvuta juu matone ya maji,Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake;

28. Ambayo mawingu yainyeshaNa kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.

29. Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu,Ngurumo za makao yake?

30. Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke;Naye hufunika vilindi vya bahari.

Ayu. 36