Ayu. 36:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Tena Elihu akaendelea na kusema,

2. Ningojee kidogo nami nitakueleza;Kwa kuwa nikali na maneno kwa ajili ya Mungu.

3. Nitayaleta maarifa yangu kutoka mbali,Nami nitampa haki Muumba wangu.

4. Kwani yakini maneno yangu si ya uongo;Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe.

5. Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu ye yote;Ana uweza katika nguvu za fahamu.

6. Hauhifadhi uhai wa waovu;Lakini huwapa wateswao haki yao.

7. Yeye hawaondolei macho yake wenye haki;Lakini pamoja na wafalme huwawekaKatika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.

Ayu. 36