Ayu. 36:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Tena Elihu akaendelea na kusema,

2. Ningojee kidogo nami nitakueleza;Kwa kuwa nikali na maneno kwa ajili ya Mungu.

3. Nitayaleta maarifa yangu kutoka mbali,Nami nitampa haki Muumba wangu.

4. Kwani yakini maneno yangu si ya uongo;Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe.

Ayu. 36