Ayu. 34:12-17 Swahili Union Version (SUV)

12. Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya,Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu.

13. Ni nani aliyemwagiza kuiangalia dunia?Au ni nani aliyemwekea ulimwengu huu wote?

14. Kama akimwekea mtu moyo wake,Akijikusanyia roho yake na pumzi zake;

15. Wenye mwili wote wataangamia pamoja,Nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.

16. Ikiwa una ufahamu, sikia neno hili;Isikilize sauti ya maneno yangu.

17. Je! Atatawala mtu aichukiaye haki hata mmoja?Nawe, je! Utamhukumia mkosa aliye na haki na mwenye nguvu?

Ayu. 34