14. Kwa kuwa Mungu hunena mara moja,Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.
15. Katika ndoto, katika maono ya usiku,Usingizi mzito uwajiliapo watu,Katika usingizi kitandani;
16. Ndipo huyafunua masikio ya watu,Na kuyatia muhuri mafundisho yao,
17. Ili amwondoe mtu katika makusudio yake,Na kumfichia mtu kiburi;
18. Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni,Na uhai wake usiangamie kwa upanga.
19. Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake,Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake;
20. Hata roho yake huchukia chakula,Na nafsi yake huchukia nyama nzuri.
21. Nyama ya mwili wake huliwa, isionekane;Na mifupa yake isiyoonekana yatokea nje.