Ayu. 32:15-20 Swahili Union Version (SUV)

15. Wameshangaa, hawajibu tena;Hawana neno la kusema.

16. Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni,Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;

17. Mimi nami nitajibu sehemu yangu,Mimi nami nitaonyesha nionavyo.

18. Kwa kuwa nimejaa maneno;Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.

19. Tazama, tumbo langu ni kama divai iliyozibwa;Kama viriba vipya li karibu na kupasuka.

20. Nitanena, ili nipate kutulia;Nitafunua midomo yangu na kujibu.

Ayu. 32