15. Wameshangaa, hawajibu tena;Hawana neno la kusema.
16. Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni,Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;
17. Mimi nami nitajibu sehemu yangu,Mimi nami nitaonyesha nionavyo.
18. Kwa kuwa nimejaa maneno;Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.
19. Tazama, tumbo langu ni kama divai iliyozibwa;Kama viriba vipya li karibu na kupasuka.
20. Nitanena, ili nipate kutulia;Nitafunua midomo yangu na kujibu.